Friday, April 25, 2014

MAKALA MAALUM

MUUNGANO WETU

African Brotherhood Foundation (ABF) ni  taasisi changa yenye malengo na  nia thabiti ya kuwaunganisha waafrika wote katika nyanja zote za kijamii, kiuchumi na kisiasa. Tunaamini kiu kubwa ya waafrika ni kuona Afrika inaungana na sio kutengana, sisi tumeamua kulisimamia suala hili ili kutimiza ndoto za waasisi  na wapambanaji wa harakati za umoja wa Afrika . Leo hii katika bara la Afrika muungano tuliokuwa  nao wa pekee ni wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Kama ilivyokua ada kila mwaka ifikapo tarehe 26 mwezi wa 4 watanzania tunakumbuka na kuadhimisha kuzaliwa kwa nchi yetu ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Nchi hii imetokana na zilizokuwa nchi mbili za wakati huo Jamuhuri ya Tanganyika na Jamuhuri ya watu wa Zanzibar chini ya viongozi wakuu wa nchi hizo ambao ni hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere rais wa Tanganyika na Hayati shekhe Abeid Aman Karume rais wa Zanzibar waliweza kuafikiana na kuunganisha nchi hizo kwa maridhiano ya hali ya juu baada hapo ndipo Jamuhuri ya muungano wa Tanzania ikaanza kutambulika  katika medani za kimataifa. Hivi sasa ni miaka 50 toka kuzaliwa kwa muungano huo na kuipata nchi yenye sifa kubwa katika mataifa mbalimbali ndani ya bara la Afrika na kote ulimwenguni. Imefikia wakati raia wa  nchi hii wanajivunia utanzania wao kufatia matunda yatokanayo na muungano wetu huu wa kihistoria.

 Kuna baadhi ya nchi ndani ya Afrika zilijaribu kuungana lakini zikashindwa kuendesha muungano wao ndani ya  muda mfupi ukavunjika mfano Senegambia uliokuwa muungano kati ya nchi za Senegali na Gambia ambao historia inaonyesha nchi hizi mbili mila zao na tamaduni zinafanana lakini walishindwa kuvumiliana na kuaminiana kwa pamoja ilikujenga muungano wao. Dhumuni ya kuendesha muungano wetu wa Tanganyika na Zanzibar ni kulinda utu wa muafrika, usalama, kukuza uchumi wa nchi hizi,  kuwezesha muingiliano wa watu wa pande zote mbili na kuifanya Afrika yetu iweze kuungana kwa pamoja ili kuepuka vita vya wenyewe kwa wenyewe.


 Tunaelewa kabisa katika muungano wetu huu kunachangamoto ambazo zinahitaji busara na hekima za watu wa nchi hii wakiwamo viongozi na raia wa kawaida kuweza kuzitatua bila ya hiyana yeyote ile. Kuna baadhi ya watu wanajaribu kuchomoza na hoja zao dhaifu na kutaka kuuvunja muungano kwa madai wamechoshwa na muungano ni bora uvunjike, sawa ni uhuru wakujielezea inaotokana na katiba ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ibara ya 18 kifungu (A), lakini tusitumie uhuru huu kwa kuwapotosha watu wa nchi hii tukifanya hivyo basi tuwe tayari historia kutuhukumu sisi na vizazi vinavyokuja. Waliopigania muungano huu hawa kuwa wajinga hata kidogo walitanguliza maslahi ya nchi kwanza na Afrika ndio maana ukapatikana muungano huu tulionao hivi sasa, hivyo tunao wajibu wa kuulinda kwa gharama yeyote ile ili muungano wetu usivunjike. 


Leo hii tunajua kabisa mwananchi wa Micheweni, Machomane, Jang’ombe hata Kilimani hawana matatizo na wananchi wa Ifakara,  Msoga, Bariadi , isipokua kuna baadhi ya watu walio wabinafsi wanataka tofauti na mitafaruku itokee sisi ni mashahidi wa yale yanayo tokea sudani ya kusini wala haya hitaji mwalimu atufundishe bali akili zetu zinafanya kazi katika kutafakuli na kuyachambua yanayo wasibu ndugu zetu wale,hivyo basi tutumie mfano ule kama funzo tosha kwetu katika kuakikisha tunalinda muungano wetu. Tukumbuke tunajivunia utanzania tuliokuwa nao kutokana na muungano wetu ,amani hii tunaoiona ni mbegu zilizopandwa 26/4/1964 na sasa tunavuna matunda ya utulivu hivyo kila mmoja wetu anao wajibu wa kuulinda muungano huu tuache porojo ambazo zitatupelekea kwenye dimbwi la machafuko wengine mkakimbilia ughaibuni mkaacha raia wanapata shida zitakazo ipoteza nchi yetu kwenye ramani ya amani na utulivu.


Sisi African Brotherhood Foundation(ABF) wito wetu kwa serikali ya Jamuhuri ya muungIano wa Tanzania waache kulewa na madaraka badala yake wasikilize kero za wananchi  na wawe tayari kuzishughulikia ili ufumbuzi  uweze kupatiana kwa urahisi. Jukumu lao kuu ni kuulinda muungano pia wanawajibu wa kulinda rasilimali zetu na kuondoa umasikini,ujinga,na maradhi itasaidia kupunguza kero za muungano kwa asilimia kubwa na kuwafanya watu kuwa wamoja na hata wale wasio utakia mema watashindwa pakuanzia. Hapa uzalendo unatakiwa ili kuupata muundo utakao leta tumaini katika muungano wetu, vilevile mnatakiwa kufanya mambo yenu kwa uwazi ili kupunguza tuhuma na malalamiko ya kila wakati kwa serikali hususani katika suala hili nyeti la muungano tujitahidi kuiga mema yaliofanywa na waasisi wa taifa hili kwani walikuwa waumini wa muungano na wapingaji wa sera za unyonyaji ndio maana walifanya jitihada kupatikana kwa muungano huu.


 Mwisho wale wanaodhani wanaweza kututenganisha wakumbuke sisi ni waumini wa muungano hivyo basi hawana nafasi yeyote ya ushawishi kwetu,kama wanaweza basi wautenganishe ule mchanga uliochanganywa  na mzee Nyerere pamoja na mzee Karume. Tusisubiri maadhimisho ya kila mwaka bali tunawajibu wa kukumbuka muungano na kuulinda siku zote za maisha yetu Afrika kwanza mimi baadae.

 
ONE BLOOD, ONE LOVE, ONE AFRICA FOREVER!

Friday, March 7, 2014

MAKALA MAALUM

MWANAMKE NI MAMA WA DUNIA


African Brotherhood Foundation (ABF)  ni  taasisi changa yenye malengo na  nia thabiti ya kuwaunganisha waafrika wote katika nyanja zote za kijamii, kiuchumi na kisiasa. Hivyo basi tunaamini kiu kubwa ya waafrika ni kuona Afrika inaungana, sisi tumeamua kulisimamia suala hili ili kutimiza ndoto za waasisi wa umoja wa Afrika  ambao nyuma yao walikuwepo wanawake katika mapambano ya kutafuta uhuru wa bara la Afrika.
Mtazamo wa  African  Brotherhood  Foundation, kama ilivyo siku zote katika dunia, mungu ameumba vitu mbalimbali kwa maana yake. Leo hii kona ya ABF Africa imeona igusie na kuelezea  juu  ya mwanamke. Kimantiki  ndani ya dunia hakuna mwanadamu asiye zaliwa na mwanamke na watu wote ni lazima tuwathamini wanawake.  Sifa za mwanamke katu hatuwezi kuzimaliza kwa maana thamani yake ni kubwa na zenye kuvutia ukizisikiliza na kuziona. Katika bara letu la Afrika wanawake wana mchango mkubwa sana. Busara zao ndizo zilichangia Afrika kuwa huru mpaka hivi sasa ingawa  wadai uhuru wa  nchi nyingi za Afrika walikuwa ni wanaume. Lakini ukitazama utaona mwanamke alikuwa nyuma ya mwanaume kwa kumpa mawazo na muelekeo mzuri ndio maana mambo yalikwenda kwa kasi na uweledi kwasababu kama tunavyo jua mwanamke akilala jamii imelala.
Hebu tazama mwanamke alivyokuwa mbunifu. Familia nyingi za bara hili la afrika zinategemea uwepo wa mwanamke ili ziweze kupata maendeleo ya mali, chakula na hata mavazi. Hii ni kwa sababu yeye ndiye chanzo cha ufanisi katika jamii kwenye kutimiza wajibu wa kila siku. Mungu aliwaumba kwa makusudio maalumu ya kuisaidia na kuikomboa jamii sio kuwa wasindikizaji kama madai ya baadhi ya watu wenye fikra potofu na mawazo mgando. Kona ya ABF Africa inapenda kuwaambia watu wanaonyanyasa wanawake waache mara moja, hivi nyie hamna huruma wala chembe ya ubinadamu hata kidogo? Mama amebeba ujazito wako miezi tisa, amejifungua kwa uchungu na kukulea kwa shida na dhiki na kufikia kipindi chakula nyumbani hakuna aliweza kutumia maarifa ya ziada kwa kuchemsha mawe ili akupe moyo na kutuliza njaa yako? Vilevile kufanya jitihada kwa kupata chakula kwa siku inayo fuata iwe kwa kukopa au njia nyingine lakini leo hii wewe binadamu usiye na huruma wala shukurani kwa mwanamke unamdharau na kumnyanyasa! Tambua amani unayo iona hii imetokana na yeye kwa sababu ndiye chanzo cha amani duniani kwa ujumla kutokana analeta utulivu na kuzuia jazba za kina baba majumbani. Leo  sisi ni mashuhuda viongozi wengi wanapendeza na kupanda majukwaani na kujinasibu ni kazi kubwa  inayofanywa na wanawake kwa utashi mkubwa waliopewa na mungu.
 Asiye mpenda mwanamke asipewe kipaumbele cha aina yeyote ile katika jamii, ushujaa wa mwanamke upo kwenye mafungu yote ya kinadharia na kivitendo. Mtazamo wa kona ya ABF Afrika ni kuona Afrika inaungana ili kukata kiu kubwa ya watu wengi wa bara letu. Hii ndio maana imeamua kumuelezea mwanamke kwa kutambua kabisa bila ya yeye kuwepo na kushirikishwa muungano tunao upigania hauwezi kupatikana bila michango yao. Na kwa kulifahamu hilo ni lazima tuwashirikishe moja kwa moja na kuungana nao kwenye harakati zao zote za mabadiliko kimaneno na vitendo.
Jamii za kiafrika zinapaswa zibadilike ili ziweze kupata maendeleo vilevile zitambue kwenye kila jambo la kimaendeleo kuna mwanamke, kona ya ABF Afrika itaendelea kulaani mateso, ukandamizaji, ukatili na unyanyasaji dhidi ya mwanamke bila ya kificho wala uwoga wa aina yeyote. Kama taasisi changa ya AFRICAN BROTHERHOOD FOUNDATION (ABF) kwa pamoja tunatambua mchango mkubwa unaofanywa na mwanamke, huu sio wakati wa kulalamika, mtumie fursa za kujenga hoja zenye mantiki na zenye kuleta mabadiliko kwenye jamii za kiafrika. Kwa maana hiyo kushirikiana na mwanamke kutaleta misingi ya uzalendo, utawala bora, umoja na mshikamano wa hali ya juu kwa bara la Afrika.
Vilevile tunatambua michango iliyofanywa na inayofanywa na wanawake katika bara hili shukrani kubwa kwa marehemu Bibi TITI MOHAMED, Mama MARIA NYERERE, Mama GRACE MACHEL, Mama WINNIE MADIKIZZELA MANDELA , Mama SALMA KIKWETE, HELLEN SELIF JOHNSON, DKT. ASHA ROSE MIGIRO, PROF ANNA TIBAIJUKA  na wengine wote kwa michango yao iliyotupelekea tupate uhuru na maendeleo ya bara la afrika. Wanawake wote hawapaswi kukata tamaa, wanapaswa kuongeza juhudi na kuunganisha maarifa yao kwa pamoja wataleta maendeleo endelevu na kulifanya bara la afrika kwenda mbele.
Wito wetu kwenu ni kuwaasa mtumie nafasi  mnazo zipata kudumisha umoja wenu pamoja na ule wa Afrika, tusisubiri maadhimisho ya kila mwaka bali tushirikiane pamoja kila wakati na kupambana na wale wote wasio watakia mema. Ni vyema kupambana nao kwa sheria ili iweze kuwa fundisho kwa wale wanao wanyanyasa wanawake na kuwanyima haki zao za msingi. Kuliko kuwaacha na kuzidi kuwafanyia wanawake matendo maovu yasio stahili katika jamii na kuzidi kuwarudisha nyuma.
Vilevile kwa upande wa serikali za Afrika zitazame kwa umakini sekta ya afya hususani kwa upande wa   wodi za wazazi. Hospitali nyingi hazina vifaa vya kutosha ukiangalia kitanda kimoja utakuta watu zaidi ya mmoja hii ina hatarisha afya ya mama na mtoto hebu tuwe na chembe ya huruma kwa hawa mama zetu, bila ya wao tusinge kuwa hapa tulipo na jamii yeyote bila ya mwanamke haiwezi kuendelea.
Serikali ina wajibu wa  kutunga sheria itakayo mlinda mwanamke na kumpa utambulisho katika jamii kutokana mila potofu zimekuwa zikimnyima haki za kimsingi kama vile kuzuiliwa kwenda shule, kutokuwa na maamuzi katika jamii. Hivyo basi ili kumsaidia mwanamke  kuondokana na manyanyaso anayoyapata kila siku hakuna asiyejua kama mwanamke anaweza kufanya mabadiliko yaletayo tija na manufaa kwa jamii zetu tumeweza kuona baadhi yao na tuna mifano ya kuwazungumzia na kujivunia uwepo wao.
Kuna umuhimu mkubwa wa kutungwa kwa sera ya kumlinda na kumtetea mwanamke. Ni jukumu la serikali na wadau kwa kushirikiana kwa pamoja. Hii itamuwezesha mwanamke kutoka kifungoni alipo kwa muda mrefu sasa bila ya hatia yeyote, hivi ni kosa kwa wao kuwepo duniani? Au wemepoteza uhalali wa kuishi? Maana tafsiri potofu za baadhi ya watu zimewafanya wanawake kuwa kama yatima waliokosa misaada ya kimaisha. AFRICAN BROTHERHOOD FOUNDATION (ABF) imeona  “ni bora kufa kuliko kuishi na hisia zilizo kufa” kwa kulikemea hili kwa nguvu moja na kutangaza rasmi uadui na wale wote wanaomtesa na kumnyanyasa mwanamke na kuzitaka jamii zote za Afrika kushirikiana katika kumkomboa mwanake kwa nguvu moja.
Mwisho, wakati wa kusimamisha haki za wanawake umefika. Afrika ni mali ya watu wote. kuheshimiana na kuvumiliana itajenga jamii ya watu wenye fikra hai zenye mashiko ndipo maendeleo yatapatikana bila ya kupiga hodi wala foleni kwa kusubiri misaada kutoka ughaibuni. Mwanamke ndiye nguzo na mustakabali wa bara la Afrika na dunia kiujumla.
One blood, One love, One Africa forever

Tuesday, February 25, 2014

AFRIKA NA JINAMIZI LA UBINAFSI.

      Ni miaka mingi sasa toka wazee wetu,wanaharakati na wanamajumui kama Mwl J.K.Nyerere, Patrice Lumumba, Kwame Nkrumah, Booker T. Washington, Marcus Garvey na William du Bois watangulie mbele za haki. Ni ukweli usiopingika kwamba kimwili hatunao tena lakini kiroho na kifikra daima wapo pamoja nasi. Hawa wote walikuwa wazalendo na wapiganiaji haki za mtu mweusi. Siku zote walitamani kuona utu wa mtu mweusi unapatikana. Wanamajumui hawa hawakua tayari kuona mtu mweusi ananyanyaswa na kuonewa. Siku zote walipigania umoja baina ya waafrika na watu weusi kiujumla na sio maendeleo yao ili wapate utukufu binafsi( self glory). Hakika wazee wetu hawa Afrika kwao ilikua ni mwanzo na mwisho (Alfa na omega). Wanaharakati hawa kwao ilikua afrika kwanza Mimi badae...

"Gharama ya kutafuta uhuru ni bora kuliko malipo ya ukandamizaji".

        Leo hii ni miaka kadhaa tangu wanamajui hawa watangulie mbele za haki. Swali la kujiuliza ni je, viongozi wa Afrika na waafrika kiujumla wanawaenzi vipi wazee hawa? Bila shaka wazee hawa hawaenziwi tena. Falsafa za wazee hawa zimetelekezwa. Waafrika kwa bahati mbaya au kwa makusudi kabisa wamepuuza falsafa na misingi ya wazee hawa. Wazee hawa wamezikwa na misingi yao ya uzalendo, umoja,mshikamano,upendo na amani baina ya waafrika.

        Ndugu zangu, wakati wazee wetu kama kina Nyerere, Lumumba, Mandela, na Nkrumah wakiamini Afrika kwanza mimi baadae, viongozi wa sasa na waafrika walio wengi wametawaliwa na mimi kwanza nchi yangu baadae na sio Afrika tena. Asilimia kubwa ya waafrika ni wabinafsi au kwa lugha nyingine waswahili wanasema "wamimi". Wengi wanajali maslai binafsi na sio maslai ya waafrika kiujumla.

"Toka siku nyingi nia ya uovu mkubwa uliopandikizwa kwetu na wakoloni wanao ondoka, na ambao tunajipandikiza wenyewe katika hali yetu ya sasa ya utengano, ilikua ni kutuacha tumegawanyika katika mataifa yasiyojiweza kiuchumi ambayo hayathubutu kupiga hatua katika maendeleo ya ukweli.............".

       Viongozi wa Afrika hawana uchungu na bara la Afrika. Uzalendo umebaki kwenye majukwaa ya kisiasa. Uzalendo kwa viongozi waafrika na waafrika kiujumla sio tena kitu cha kujivunia. Ukosefu wa uzalendo kwa waafrika kumepelekea kuongezeka kwa rushwa Afrika, njaa, vita za wenyewe kwa wenyewe, elimu duni, magonjwa na umasikini ulio kithiri. Inasikitisha sana kuona bara la pili kwa idadi kubwa ya watu, bara la pili kwa ukubwa na bara lenye utajiri mkubwa wa rasilimali duniani linaendelea kuwa tegemezi na maskini.

         Ubinafsi kwa viongozi umepelekea wasaini mikataba mibovu yenye kuwanufaisha wao wenyewe, wajilimbikishie mali na wengine kuthubutu hata kuhamishia fedha zao kwenye akaunti za siri huko ughaibuni. Wakati viongozi wakifanya haya watoto wa shule wanakaa chini (sakafuni), shule hazina vitabu vya kutosha wala maabara. Wakati vijana wafrika wanashindwa kuendelea na masomo kwa kukosa mikopo ya vyuo vikuu, viongozi wa Afrika wameendelea kuona fahari kusafiri kwenda nchi za ulaya wakijua ndio fursa pekee ya kupiga picha na kushikana mikono na maraisi na mawaziri wakuu wa nchi kubwa zinazojiita zimeendelea.

Kwa upande mwingine waafrika ambao sio viongozi lakini wanao uwezo kifedha nao wanasakamwa na jinamizi la ubinafsi. Inasikitisha kuona matajiri wa Afrika wanatumia fedha nyingi kufadhili vyama vya siasa na wanasiasa lakini wengine wakithubutu kuwaruhusu mashabiki wa mpira wa miguu waingie bure katika viwanja kisha gharama zote atalipa yeye, lakini waafrika wangapi pale Amana hospitali wanachangia kitanda? Watoto wa shule wangapi Afrika wanakaa chini kwasababu ya ukosefu wa madawati? Kwanini hizo fedha wasiwasaidie waafrika hawa? Au kwasababu waafrika hawa wa kawaida hawana uwezo wa kutoa misamaha ya kodi kwa makampuni yao? Matajiri wakubwa wa Afrika lazima muache ubinafsi, vinginevyo Afrika itaendelea kuwaita maskini.

Inasikitisha sana kuona baadhi ya waafrika wapo tayari kutoa fedha nyingi kuwatunza waimbaji na wanenguaji wa bendi za muziki bila kujiuliza mara mbilimbili ili mradi tu wanamziki hawa wawaite "pedezyee fulani". Wakati mapedezyee hawa wakifanya hivyo,kuna waafrika Somalia wanakufa kwa njaa, vijiji kule Botswana havipitiki kwa ubovu wa barabara,waafrika katika hospitali ya Muhimbili Tanzania wanakufa kwa kukosa matibabu. Je,wanasubiri waafrika hawa waite "pedezye..." Kama wafanyavyo wanamuziki ndio wapeleke vitanda kule hospitali ya Peramiho Songea? Au madawati kule shule ya msingi Katubuka Kigoma? Waafrika mnaojiita mapedezye lazima mbadilike lasivyo Afrika itaendelea kutegemea mataifa ya kibepari wakati sisi wenyewe tukiamua tunaweza kuliendeleza bara letu.

Mwisho ningependa kutoa wito kwa waafrika wote waige mfano wa Booker T Washington aliyeamua kujitolea kujenga shule takribani 500, 'railway' kule Virginia na kuanzisha miradi mbalimbali kwajili ya kumkomboa mtu mweusi kule Marekani pasipo kuingojea serikali. Hivyo waafrika wote tuchukue jukumu la kuliendeleza bara letu bila kujali tofauti zetu za kidini, kikabila,kisiasa na kitaifa na sio kuziachia serikali peke yao.

"Afrika kwanza Mimi badae...."


One blood, one love, one Africa forever...

Friday, February 7, 2014

VIONGOZI KATIKA BARA LA AFRIKA


Kwenye kumbukumbu zangu hili neno uongozi sio suala geni hata kidogo. Kwa upande mwingine kila siku katika jamii zetu huwa tunasikia watu mbalimbali wanazungumzia yanayo husiana na uongozi kwa kutaja muhusika au wahusika wa uongozi ambao ni kiongozi au viongozi. Vilevile watu wanatafsiri neno uongozi kwa maelezo tofauti tofauti ili wapate maana.

Kona ya abfafrica inatafsiri na kuelezea maana ya uongozi; Uongozi ni dhana, taaluma inayompa muhusika madaraka, mamlaka na uwezo wa kuwawezesha wale anaowaongoza kuunganisha nguvu, ustadi na kuvitumia vipaji vyao ili kufikia malengo yao kama ni kiuchumi, kijamii ama kisiasa. Katika uongozi kuna aina ya uongozi, kama vile wakurithishana ambao mara nyingi ni utawala wa kifalme unaoendeshwa kwa njia ya urithi. Aina nyingine ni uongozi wa kuchaguliwa na watu ambao hutumia fursa ya kupiga kura kupitia chaguzi mbalimbali. Uongozi wa kimabavu daima yule mwenye mmlaka anaendesha utawala ule kwa mawazo yake bila ya kushirikisha watu anao waongoza bila ya kufuata misingi ya haki. Uongozi wa kuteuliwa na mamlaka za juu mfano raisi kumteua balozi, jaji, mkuu wa majeshi.


Kona ya abfafrica leo inapenda kuelezea juu ya uongozi wa Afrika ili kuipa jamii ya watu wa Afrika fursa ya kutambua viongozi wao waliowachagua na namna wanavyoendesha nchi zao. Uongozi bora ni ule unao simamia misingi ya utu, wenye kulenga maslahi ya watu, kutetea haki za binadamu, kuleta usawa bila ya kujali dini ama kabila la mtu. Pia viongozi wanapaswa kuwa watu wenye maadili mema yenye kulenga na kufuata taratibu na mwenendo wa kiafrika, kusimamia rasilimali za watu wanaowaongoza, kutetea watu wake na kuwapigania kwa nguvu moja, na kuwaunganisha watu wake na jamii zinazo wazunguka. 
"Ni vizuri kuongoza ukiwa nyuma na kuwaweka wengine mbele, hasa mnapo sherehekea ushindi na wakati mambo mazuri yanapotokea. Na kukaa mstari wa mbele wakati kuna hatari. Kwa kufanya hivyo, watu watauheshimu uongozi wako.
Nelson Mandela."

Swali linakuja, je, viongozi wa Afrika wanafanya haya?. Historia ya bara letu la Afrika inatuonesha namna viongozi waliopita walivyo kuwa na kiu kubwa ya kulifanya bara hili liwe moja ndio maana tarehe 25 mwezi 5 mwaka 1963 sahihi za viongozi 32 walioketi pale mjini Addis Ababa katika nchi ya Ethiopia, chini ya mwenyekiti wa kwanza hayati HAILLE SELASSIE 1, kiongozi mkuu wa Ethiopia wa wakati huo lengo ni kuinganisha Afrika katika masuala ya umoja na mshikamano wa nchi za Afrika na kuweza kuwa na sauti moja ya bara la afrika. Vilevile kuinua hali ya kimaisha ya waafrika waliotoka ndani mikono ya wakoloni, Vilevile walitaka kusaidia nchi zote zilizo kuwa bado hazijapata uhuru kuhakikisha zinakuwa huru. Mfano wa nchi hizi ni ZIMBABWE,AFRIKA YA KUSINI, ANGOLA nk. Ukitazama kwa undani viongozi wale kikubwa walichokitaka ni kufanya muungano wa kihistoria utakao lenga kupata Afrika moja.
"Mpaka itikadi inayolifanya tabaka fulani kuwa juu na jingine kuwa chini kuondolewa na kutokomezwa, kila sehemu  itakua ni vita na mpaka pale ambapo hakutakua na raia wa daraja la kwanza na wale wa daraja la plili katika taifa lolote, mpaka rangi ya ngozi ya mtu haitakuwa na tija kuliko rangi ya macho yao. Na mpaka haki za binadamu zitakapo zingatiwa kwa wote bila kujali rangi, vita itakuwepo. Na mpaka ile siku ambayo, ndoto ya amani ya kudumu, uraia wa dunia, uongozi wa maadili ya kimataifa, itabakia kuwa ndoto ya kusadika inayohitajika kutimizwa na kamwe haijafikiwa, sasa kila sehemu ni vita" Haile Selasie 1

Hata hivyo kona ya Abfafrica imebaini kuwa viongozi waliopita walifanya jitihada zao za dhati kwa ajili ya watu wao wa Afrika. Ukiangalia namna walivyo pambana na wakoloni nakuweza kuwatoa vilevile kwa kutuonesha njia ya muungano wa bara la Afrika. Leo hii viongozi walio wengi kati ya hawa tulionao wanashindwa kutimiza na kutekeleza majukumu yao kutokana wamekuwa vibaraka wa nchi za magharibi. Hii ni aibu kubwa! Hebu tazameni raia wenu wa bara hili wanavyopata tabu na kusumbuliwa huko ugaibuni! Hivi hii ndio Afrika ambayo JK Nyerere na Kwame Nkurumuah waliyo tuachia? Kumbukeni watu walijitoa sadaka kwa ajili ya bara hili. Daima tuwe tunakumbuka na kusoma historia ya nyuma. Na hivi vinavyo endelea sasa ni dhambi ya ubaguzi na unafiki tulizonazo miongoni mwetu. Tufikirieni kwa umakini wa hali ya juu kwa mitazamo chanya ili tuweze kupiga hatua. Hebu tazama hapa imefikia hatua baadhi ya vijana wa Afrika wanatamka maneno haya "Ni bora wangezaliwa mbwa Ulaya kuliko kuendelea kuishi afrika" hii sio lugha nzuri hata kidogo, ninaweza kusema ni ya kipuuzi. Lakini yote haya yanasababishwa na viongozi wetu wa Afrika kwa kushindwa kutekeleza sera zetu na kumthamini sana mtu wa nje ya bara hili. Chonde chonde viongozi wangu hebu acheni mara moja utumwa huo.

Afrika ina idadi ya watu wanakadiriwa kufika bilioni 1.033 kwa takwimu za mwaka 2013. Hebu viongozi wangu waleteni pamoja watu hawa ili tuzidi kuimarika kiuchumi. AFRICAN BROTHERHOOD FOUNDATION  ina malengo ya kukutana na viongozi wote wa Afrika ili iwakumbushe na kuweza kujitathimini tulipotoka, tulipo na tunapokwenda. Inawezekana baadhi yao ulevi wa madaraka umewalevya na kushindwa kukumbuka yale yote yalio pita. Vilevile inawataka watu wasijinasibishe kwa nchi walizo toka tu, bali ni vyema zaidi kujivunia Afrika kwasababu wote asili yetu ni moja na haiwezi katu kupotea hii ni ngao yenye upeo wa harakati zetu zilipotokea hivyo hatuna budi kujivunia na kujitukuza kabla ya kutukuzwa kwa maana hiyo afrika ni moja bila ya shaka tunapaswa kujivunia afrika yetu. 

Viongozi wote tunawaomba msiende makao makuu ya Afrika pale Ethiopia ilimradi muonekane mmeenda bali nendeni pale kwa lengo la kuutaka umoja wa Afrika una hakikisha maendeleo ya Afrika yanapatikana na maazimio yake yote yanatimizwa kwa wakati. Hii itatusaidia watu wote turudishe imani kwenu kama viongozi wetu kwasababu mtazuia wimbi kubwa la vijana lisikimbilie ugaibuni na nguvu kazi ya Afrika ikazidi kupungua. Hii italifanya bara hili kuweza kukua kiuchumi na kustawi zaidi katika ramani ya dunia.

Kuna baadhi ya viongozi wanatoka ugaibuni wanakuja Afrika kama ukiwasikiliza maneno yao, ni ya kuwakatisha tamaa waafrika wasiungane kwa sababu hilo ndio lengo lao kubwa kwa kuwa Afrika ikiungana hakuna tena gesi, mafuta, wala madini ya bure. Hivyo adui wao mkubwa ni muafrika anayejitambua na rafiki yao mkubwa ni muafrika muoga na mwenye kuzembea harakati za Afrika. 

Kona ya Abfafrica inaona ajabu sana kuona baadhi ya viongozi wa afrika wanaona wanapendwa na wale viongozi wa magharibi kumbe wanatumiwa tu kama karatasi. Napenda kuwakumbusha wako wapi akina Savimbi wa Angola na Mabutu wa Zaire? Wakishakutumia watakumaliza tu! Ombi langu kwenu tuache mara moja kuwa vibaraka, tuitazame kwanza Afrika. 

Bila ya kufanya hivyo kazi tulioachiwa na waasisi wa umoja wa Afrika, ambayo kazi kubwa ni kuhakisha Afrika inaungana na kuwa moja, maendeleo makubwa ya Afrika hayato patikana mpaka tuungane kwa ukweli. Matendo yanahitajika sana kuliko maneno. Mwendo mzima wa Afrika unapaswa uendeshwe na waafrika wenyewe. Tunamshukuru Mungu kwa kutujaalia rasilimali za kutosha vilevile kuweza kutupatia wataalamu wa fani mbalimbali hivyo basi ni jukumu kubwa la viongozi na uongozi wote wa Afrika kwa ujumla wake kuwatumia na kuwaleta pamoja watu wake. 


Mungu ibariki Afrika. One Blood, One Love, One Africa, Forever!.





Wednesday, January 29, 2014

SUDANI YA KUSINI: Machar asema tuhuma za mipango ya mapinduzi hazina "mashiko".

Ramani ya vita Sudani ya Kusini.

Kiongozi wa waasi Sudani ya Kusini ameiambia BBC tuhuma za mapinduzi juu yake na baadhi ya washirika wake hazina mashiko.

Bwana Machar ambaye kwa sasa yupo katika harakati za kukimbia amesema anategemea wajumbe katika mgogoro huu watahakikisha washirika wake wanne waliofungwa wanaachiwa.

Wachambuzi wanasema suala hili linatishia mkataba wa amani ulio sainiwa wiki iliyopita.

Mwezi Disemba Maofisa walitangaza  kwamba wanasiasa saba wanatuhumiwa kufanya jaribio la mapinduzi.

Mwanzo ulikua ni mgogoro wa kisiasa kati ya rais Salva Kiir na makamu wake wa zamani Bwana Machar tarehe 15 Disemba.

Kuanzia hapo vurugu zilianza zikapelekea vita kubwa na imeripotiwa kutokea mauaji ya kikabila.

Wanasiasa saba maarufu waliokuwa wakikiongoza chama cha SPLM walikamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi mara tu baada ya madai ya kutaka kufanya mapinduzi.

katika wanasiasa hao wanne wanatuhumiwa kufanya mapinduzi na wengine saba wameachiwa katika mamlaka za Kenya ambapo walionekana wakiwa na Rais wa Kenya Uhuru Kenyata katika mkutano wa habari hapo siku ya Jumatano.

Zaidi ya watu 646,000 wamepoteza makazi toka mapigano yaanze mwezi Disemba.

Wednesday, January 22, 2014

PIGO KUBWA KWA AFRIKA BAADA YA KUMPOTEZA MWANAHABARI WETU MAHIRI, KOMLA DUMOR

Komla Dumor

Imeripotiwa; Mwanahabari wa BBC TV, Komla Dumor 41, amefariki ghafla katika nyumba yake iliyopo London.

Ni mzaliwa wa Ghana, alikuwa ni mtangazaji wa habari za BBC za dunia haswaa katika habari za Afrika.

Mtangazaji huyu alikua ni maarufu duniani, alijiunga na BBC kama mrusha matangazo ya redio mwaka 2006, baada ya kuwa mwanahabari kwa muda wa muongo mmoja huko Ghana.

Rais wa Ghana ametangaza kupitia Twitter kwamba nchi yake imepoteza moja ya "mabalozi mahiri".

Mkurugenzi wa habari za dunia BBC Peter Horrocks amemuita Komla Dumor mwongozo wa wanahabari wa Afrika  ambaye atakumbukwa sana kwa mchango wake.

"Alidhamiria kuelezea habari ya Afrika kama ilivyo" Bwana Horrocks alisema katika tamko.

"Furaha na nguvu ya Afrika huonekana kuongezeka katika kila habari aliyo eleza Komla".

"Ndugu na marafiki katika Afrika yote watakuwa na huzuni kama tulivyo sisi katika habari hii ya kuhuzunisha".

BBC imekua ikielewa kwamba Komla alikuwa akiumwa ugomjwa wa moyo.

Katika jarida la New African's magazine, la Novemba 2013, Komla alikua katika orodha ya watu 100 wenye ushawishi katika bara la Afrika. Lilisema "Komla amekuwa ni uso wa Afrika katika habari za ulimwengu na amekua na ushawishi mkubwa katika jinsi gani tunaifikia Afrika.

Komla Dumor alikua na ujuzi na mbinu za kuvutia katika utangazaji.
 James Harding, mkurugenzi wa habari na mambo ya sasa, akiongelea "jukumu pekee la Komla Dumor katika kuifikia Afrika". Alitumia uelewa, ujasiri wa hali ya juu, furaha yenye kuvutia na mvuto kwa watu katika kazi yake.

Komla Dumor alizaliwa tarehe 3 Octoba 1972 huko Accra Ghana.

Alipata bachela ya socialogy na saikolojia katika chuo kikuu cha Ghana na masta ya public administration katika chuo kikuu cha Havard.

Alipata tuzo ya mwana habari bora wa Ghana mwaka 2003 na miaka miwili baadae alijiunga na BBC.

Kuanzia hapo mpaka alikua akitangaza kipindi cha Network Afrika katika redio ya BBC world service kabla hajajiunga katika kipindi cha World Today

Komla Dumor akitangaza kipindi cha African Business Report mwaka 2009.

Mwaka 2009 Komla akawa mtangazaji wa kwanza wa kipindi cha African Business report katika habari za ulimwengu za BBC.  Pia alikua mtangazaji wa kipindi cha Focus on Africa na alifanya kazi hiyo siku moja kabla hafariki.

Alitembelea sehemu nyingi za Afrika akikutana na wajasiriamali maarufu na kuripoti mambo ya biashara yanayo endelea katika sehemu mbalimbali za baa la Afrika.

Alifanya mahojiano na wageni wa hadhi ya juu kabisa hii ni pamoja na Kofi Annan na Bill Gates.

Mwezi uliopita, alishughulika katika kutaripoti mazishi ya rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, ambaye alimwelezea kama "moja ya watu maarufu katika historia ya sasa."

Alifanya matangazo ya moja kwa moja ya matukio makubwa kama kombe la dunia la mwaka 2010 huko Afrika Kusini, mazishi ya Kim Jong-il, kuachiwa kwa mwanajeshi wa Izrael Gilad Shalit, na ndoa ya mtoto wa mfalme, William na Kate Miidleton.

Katika mjadala wa 2013 uliochapishwa mwezi jana, Dumor alisema kufariki kwa Mandela ni "moja ya vipindi vitakavyobaki na yeye".

"Kuripoti mazishi kwa mimi kumekua na kutaendelea kuwa tukio la kipekee. Taliangalia tukio hili kwa hali ya huzuni na kwa shukrani na heshima. Najiona mwenye bahati kuwa shahidi katika sehemu ile ya historia ya Mandela".

"Hajawahi kuterereka!"

Kukutana n Komla Dumor kwa mara ya kwanza mwaka 2007, mkuu wa watoa habari wa kimataifa Lyse Doucet algundua ni kwa jinsi gani mwanahabari huyo alionekana kwake.

Hajawahi kuwa muoga katika kuuliza mwaswali magumu, pia alipenda kufurahi na wengine, alisema.

Aliongeza kuwa Komla Dumor alikua na vitu vingi alivyokua napenda kama soka, imani yake na familia yake.

Ameacha mke na watoto watatu. 



Sunday, January 19, 2014

MGOGORO WA JAMHURI YA AFRICA YA KATI: MIILI YACHOMWA HADHARANI

Thomas Fessy akiripoti kutoka Bangui: Kutokuwepo kwa serikali,
sasa magenge yenye hasira yanaongoza mitaa

Genge la wakristo limewaua na kuwachoma waislam wawili huko Bangui, Jamhuri ya Afrika ya Kati. Hii ni katika mzozo wa kidini unaoendelea.

Genge hilo la majambazi limeiambia BBC kwamba litaendelea kuwaua waislam katika eneo lao.

Majeshi ya Umoja wa Afrika na Ufaransa yanajitahidi kudhibti hali ya mgogoro huo wa kiitikadi za kidini ambao ulizuka mara baada ya kundi kubwa la waasi wa kiislam kuchukua na kudhibiti nchi.

MP wanaelekea kuchagua rais wa mpito ifikapo Jumatatu wiki moja baada ya kiongozi wa waasi Michael Djotodia kuachia madaraka.

Rais huyu alitwaa madaraka baada ya kundi lake la waasi kuipindua nchi mwezi Machi mwaka jana.

Mapinduzi haya yalipelekea kuibuka kwa mgogoro wa kiitikadi za kidini kati ya wakristo wengi na waislam ambao ni wachache.

Bwana Djotodia alijiuzulu tarehe 11 January baada ya kushindwa kutuliza machafuko.

Ingawa ilionekana machafuko kama yanatulia baadaya kujiuzulu lakini imeripotiwa kutokea vurugu zaidi baada ya wiki kupita.

Ijumaa, wakala wa msaada wa afya wamesema kuwa watu wasiopungua 22 wameuliwa katika msafara wa kuwahamisha waislam kulekea Cameroon. 
Watoa msaada wa afya wakiharakisha kuiondoa miili ya waislam waliochomwa.

Genge hilo la wakristu lilimwambia Thomas Fessy wa BBC kuwa wanalipiza kifo cha mkristu mwenzao kilichotokea usiku wake. Haijulikani kama walio uawa wanahusika au wamekua walengwa kwa sababu tu ni waislam.

Baraza la Umoja wa Mataifa limethibitisha kupelekwa kwa vikosi vya Ufaransa huko CAR katika mpango wa kurejesha hali ya utulivu na hatimaye kufanyika uchaguzi kabla ya mwaka 2015.

Jumapili, bunge la mpito limetoa orodha ya wagombea nane wa urais wa mpito.

Maofisa wanasema wagombea wametimiza vigezo, mfano, hawatakiwi kuwa wanachama wa  kundi la kivita na wawe hawajawahi kufanya kazi na Djotodia wala kundi lake la waasi wa Seleka.

Katika wagombea hao yupo Meya wa Bangui na watoto wawili wa marais wa kabla, Sylivian Patasse na Desire Kolingba.




WAKIMBIZI KATIKA BARA LA AFRIKA


Suala la wakimbizi sio suala geni kwenye vichwa vya watu wengi. Leo kama kawaida kona ya Abfafrica imeona imulike kwa kuweza kudadavua juu ya suala la wakimbizi. Kwanza kabisa kwa kutoa maana ya neno lenyewe.


 Mkimbizi ni nani?

Ni mtu au kundi la watu waliolazimika kukimbia nchi yao ili kuepuka manyanyaso, vita au vurugu. Wakimbizi huwa na hofu ya manyanyaso kutokana na rangi, dini, uraia, msimamo wa kisiasa au uanachama katika kundi fulani la kijamii. Vita na vurugu za kidini na kikabila vimekua chanzo kikuu cha wakimbizi kukimbia nchi zao.

Kuna idara maalumu iliyoanzishwa na umoja wa mataifa yenye lengo la kusimamia wakimbizi. Idara hii ni (UNHCR). Katika bara letu la Afrika nchi nyingi zenye amani zinakabiliwa na changamoto ya wakimbizi. Mfano; TANZANIA,KENYA,UGANDA,AFRIKA YA KUSINI nk. Nchi wanazotoka wakimbizi ni pamoja na Somalia, Sudan ya Kusini, Jamuhuri ya kKdemokrasia ya Kongo, Afrika ya Kati nk.  

Shirika la Umoja wa  Mataifa la Kuhudumia na Kutetea Haki za Wakimbizi

         Idara inayo shugulikia masuala ya wakimbizi (UNHCR) imeweza kutoa takwimu za idadi ya wakimbizi kwa nchi za kusini mwa jangwa la Sahara. Takwimu zinaeleza kwamba watu millioni 3.1 kwa mwaka 2012 na idadi imeongezeka kwa mwaka huu wa 2014 kwakufikia watu millioni 3.4. Watu waliopotea inakadiriwa kufikia millioni 5.4 kutoka maeneo ya nchi za Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Somalia, Sudan ya Kusini, na Mali. Vilevile watu wapatao millioni 11 wamekosa makazi. Nchini Somalia watu wanaokadiriwa millioni 2 hawana makazi na wakimbizi millioni 1 wapo maeneo ya nchi za jirani kama vile Kenya, Uganda na Tanzania. Kutoka nchini Afrika ya kati ripoti zinaonesha watu takriban 100,000 wamekimbilia nchini Cameroon  kutafuta hifadhi. 


        Mambo  yanayo sababisha wakimbizi.
  • Vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vinaweza kuwa vya kidini, kikabila na hata uasi katika jeshi. Athari zake ni kubwa sana katika jamii. Kona ya Abfafrica imebaini asilimia kubwa ya wakina mama na watoto wanapoteza maisha kutokana na suala hili. Mfano mzuri angalia nchi ya Somalia na Sudan ya Kusini, watu na jamii zao wanakumbwa na umasikini pamoja na njaa. Pia ukosefu wa elimu unatokea hali ya kuwa uchumi unazidi kuporomoka kwa kasi kubwa. 
Wananchi wakikimbia Kongo baada ya mapigano kuzidi. Oct 2008.

  • Sababu nyingine ni umasikini na njaa unapelekea watu kukimbia nchini zao. Hebu angalia nchi ya Eritrea pamoja na Ethiopia, raia wao wanakimbilia nchi nyingine. Mfano wakati wa mashindano makubwa ya kimichezo kama vile kombe la mataifa ya Afrika, kombe la Afrika mashariki na kati, baadhi ya wachezaji ambao ni raia wa nchi hizo huwa wanatoroka katika kambi za timu zao za taifa.

  • Mapinduzi ya umwagaji damu ambayo hufanywa na wanajeshi hupelekea asilimia kubwa kukimbia nchi zao. Tuliona kipindi cha Mabutu nchini Zaire na hata Liberia, Sierra Leone, Somalia na Mali. Na hapa utasikia juu ya uvunjifu wa haki za binadamu hususani watu wanapata sana mateso kama vile kubakwa na mauaji ya kimbari. 
Baada ya kutazama vitu  hivyo, kona ya Abfafrica tukiwa kama wadau na waumini wazuri wa harakati za Afrika, tunasikititishwa sana kuona Afrika kila mwaka kunatokea matukio yanayo pelekea wakimbizi. Katika suala hili la msingi kuna vitu vinaonekana kabisa kama wa Afrika tukiamua, inawezekana vikawa historia kwa kuweza kuvikomesha mara moja. Hivi ni kwanini waasi wanazidi kushika hatamu katika bara letu? Kwani hawa hatuwajui ni akina nani na wametokea wapi? Swali hili lina jibu kabisa ndani ya vichwa vya watu wote wa bara letu hili kwa kuonesha msisitizo. Hawa waasi hawatutakii heri katika bara letu ni vibaraka tu. Hebu kwa pamoja viongozi wote wakuu wa nchi zetu za Afrika, kaeni chini mtafute njia ya kuwadhibiti hawa na wapate fundisho la milele. Waasi humaliza nguvukazi ya bara hili na hutorosha rasirimali zetu. Sisi kama wapinzani wao hebu tujitolee kuwaondoa mara moja maana ndugu zetu ambao ni wakimbizi wanapata tabu. Hebu vuta taswira na kumuangalia mama yule mjamzito na mtoto mgongoni wanavyopata tabu, halafu, je, tulitafuta uhuru wa nchi za Afrika kwaajili ya waasi? Sasa wewe kama mwana wa Afrika unasababu gani ya kuunga mkono au kuwafumbia macho waasi.

Watu walio wengi wa Afrika hatuna roho za kinyama wala za kikatili ambazo daima zinabomoa mshikamano wa nafsi na imani. Hivyo basi hatuna haja sisi kama waafrika kuwanyanyasa wala kwafukuza wakimbizi wanapokimbila katika nchi zetu kutafuta hifadhi   kwasababu tukumbuke wengi wao wanakuwa wamepoteza ndugu na jamaa zao. Hivyo hatuna budi kuwapokea na kuwasaidia kwa moyo mmoja kwa kuwapa faraja itakayo wapa matumaini katika maisha yao. Tusipo wathamini hawa ndugu zetu waafrika wenzetu,  tutamkimbilia kwa nani siku matatizo yakigeukia upande wetu. Kumbukeni ardhi ya Afrika ni mali ya waafrika. Wakoloni waliligawa bara hili kwa maslahi yao wenyewe. Hivyo hatuna budi kufuata sera za kikoloni tusiwe watu wa kuiga kutoka kwa yale mabeberu yasiyo na hata chembe ya huruma kwa binadamu wenzao. 

Ombi langu kwa umoja wa Afrika (AU) wakae chini na watathimini kwa kiwango kipi wanaweza kuwaleta waafrika pamoja. Kwa sababu ukipima kwa undani mambo yanayo tokea maeneo yenye fujo na vita kwa sauti moja yanaweza kupatiwa ufumbuzi. Kikubwa hapa ni kulitazama bara la Afrika na mwenendo wake. Kipimo cha hicho ni kulileta na kulifanya bara liweze kuwa na utawala bora, uwajibikaji, usawa, haki, demokrasia ya Afrika na maadili mema kwa watu wa Afrika. Hivi ni miongoni mwa vitu ambavyo vikikosekana katika taifa fulani basi ile hali ya amani iliyokuwepo inaweza ikapotea wakati wowote. 

Kona ya abfafrica itaendelea kulisemia hili mpaka ufumbuzi wake upatikane. Vilevile tunapenda kuwashukuru wale wote wanao wasaidia hawa wakimbizi kwa kuwapa hifadhi. Sisi AFRICAN BROTHERHOOD FOUNDATION kazi yetu ni kuhakisha watu wote wa Afrika wanapata dira na mwanga katika maisha yao, na lengo kuu ni kuona Afrika inakuwa kitu kimoja na hii ndio ndoto za ndugu zetu wakimbizi pamoja na wananchi wengine wa bara hili.  Kwa ujumla wetu tukalikabili hii itatusabishia amani kurudi mara moja na kila mtu katika bara hili akajiona yupo sehemu ya salama na sauti moja ya waafrika itarudi, hii ndio kiu kubwa inayo tuandama katika jangwa hili ambalo amani yake imekuwa ikitoweka siku hadi siku. 

Waafrika sisi wenyewe tunaweza bila ya kuwezeshwa na wahisani kutoka nje. Inatupasa wenzetu wakimbizi wanavyo pata tabu na sisi tuguswe kwa namna moja ama nyingene na kwa mtazamo huu tutaweza kusaidiana kwa hatua zote tutakazo fikia. Kama ilivyo desturi yetu Afrika itajengwa na muafrika mwenyewe na kama kuibomoa tutaibomoa wenyewe. 

Narudi tena kwa hawa waasi. Hivi leo hawa jamaa wanafikiria watamuongoza nani kama wanazidi kuwaua watu wasio na hatia. Kikubwa, hawa inawezekana kabisa kuna baadhi ya serekarli zinawapa ufadhili kwasababu wana nguvu kubwa ya silaha, wamezitoa wapi? Na kwanini wanakimbilia kwenye rasirimali? Hawa wapo chini ya udhamini wa watu wasio tutakia maendeleo leo. Kwa kauli moja tunasema tena hawa ni vibaraka wa maadui wa bara la Afrika na watu wake! Shime shime viongozi wa Afrika hebu tuoneshe uzalendo kwa bara hili. Mungu ibariki Afrika!
One blood, One love, One Africa, Forever.












Saturday, January 18, 2014

JESHI LIMEFANIKIWA KUDHIBITI TENA MJI MUHIMU WA SUDAN

Bor, mji muhimu wa Sudan ya Kusini umedhibitiwa tena na wanajeshi.

wanajeshi wakifurahia ushindi katika mi wa Bor, mji ambao umebadilishwa udhibiti mara kadhaa.
Jeshi la Sudan ya Kusini limeripoti kuwa limeukamata na kudhibiti mji muhimu wa Bor kutoka kwa waasi.

Jeshi la Uganda limesema limesaidia katika oparesheni hiyo. Msemaji wa waasi anasema uamuzi wa kuondoka ulikua ni wa busara. Bor, mji mkuu wa jimbo la Jonglei, kwa mara kadhaa umekua ukikaliwa na madaraka katika kipindi cha mwezi mmoja wa machafuko. Machafuko ambayo inaaminika yamepelekea maelfu kupoteza maisha.

Kwa wakati huo huo, mazungumzo ya kujaribu kuacha mapigano yanaendelea huko Ethiopia.

Kutokuelewana kati ya waasi na serikali kulianza tarehe 15 Disemba. Rais Salva Kiir alimshuku makamu wake wa zamani Riek Machaar kwa kujaribu kufanya mapinduzi, kitu ambacho Riek alikataa.
Mamia ya maelfu wamepoteza makazi yao wakati wa machafuko.









Bwana Kiir ni mtu wa jamii ya Dinka ambayo ni kubwa hapo nchini, wakati bwana Machar ni mtu wa jamii ya Neur. Mamia ya maelfu ya watu wamehama makazi yao katika kipindi cha machafuko.

Chanzo bbc.co.uk.

Saturday, January 11, 2014

Mgogoro wa Jamhuri ya Afrika ya Kati: Wageni wasiokuwa na makazi kuondolewa.

Kambi ya muda inayohifadhi watu wanaokadiriwa kufikia 100,000 wasiokua na makazi katika uwanja wa ndege wa Mpoko, Bangui.

Awamu ya kwanza ya kuhamishwa kwa dharura kwa maelfu ya wageni waliokimbia machafuko katika Jamhuri ya Afrika ya Kati imeanza leo Jumamosi.

Shirka la kimataifa la uhamiaji (IOM) limesema litaanza kuwasafirisha watu 800 wa Chad  kutoka kwenye kambi ya muda huko Bangui.

Raisi wa mpito wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Michael Djotodia alijiuzulu Ijumaa kutokana na maigano kati ya wapiganaji wa kiislam na kikristo.



Bwana Djotodia, raisi wa kwanza muislam, aliyepata madaraka mwaka uliopita. Toka hapo 20% ya watu wamelazimika kukimbia ili kuepuka vurugu.

Watu wasiopungua 1,000 wamefariki toka machafuko yaanze mwezi December.

Kwa sasa umoja wa Afrika ina watunza amani 4,000 ndani ya nchi. Sambamba na hilo Ufaransa inapeleka vikosi 1,600 kwenda kujaribu kurejesha amani.



Kiongozi wa umoja wa mataifa ametoa tahadhari ya kutokea majanga makubwa ya kiubinadamu.

Bofya hapa kwa taarifa zaidi.

Chanzo BBC.

Mgogoro wa Sudani ya Kusini: UN yatoa wito kwa serikali kuwaachia wafungwa

Baraza la usalama la umoja wa mataifa limemuomba rais wa Sudani ya Kusini Salva Kiir awaachie wafungwa wa kisiasa ili kusaidia katika kuhitimisha machafuko yanayoendelea. 



Kiongozi wa waasi, Riek Machar, anataka watu kumi na moja waachiwe huru kabla ya makubaliano ya amani kufanyika.

Vikosi vya Machaar vinaonekana kuzidiwa nguvu baada ya kupoteza mji wa Bentiu na kuchukuliwa na majeshi ya serikali katika siku ya Ijumaa.

Serikali inasema inapeleka maelfu ya vikosi ili kudhibiti Bor - mji mkubwa na wa mwisho unaodhibitiwa na vikosi vya waasi.

Machaar, makamu wa raisi aliyefukuzwa kazi, ameonesha nia ya kuendelea kudhibiti mji huo ambao upo umbali wa km 200 kaskazini mwa mji mkuu wa Juba.



Akiongea na AFP kwa simu, wakala wa habari, aliyejaribu kueleza tukio la waasi kupoteza mji huo:
"Ilikua ni kuepuka mapigano katika mitaa na kulinda maisha ya raia," alisema.

Msemaji wa jeshi  Philip Aguer amesema baadhi ya wapiganaji wa pande zoe wamepoteza maisha.

Pamoja na serikali kuingia katika mji huo, maelfu ya watu wameihama Bentiu, na maelfu kadhaa ya watu wametafuta hifadhi katika kambi ya UN hapo mjini.

Kwa taarifa zaidi endelea hapa.

Chanzo www.bbc.co.uk/news

Vikosi vya Sudani ya kusini vimefanikiwa tena kudhibiti mji muhimu wa Bentiu.

Andrew Harding wa BBC ameripoti kuwa ineonakana Bentiu ilidhibitiwa kutoka kwa waasi kukiwa na "upinzani mdogo tu."

 Jeshi la Sudani ya Kusini linasema wamefanikiwa kudhibiti tena kitovu cha mafuta Bentiu, mji ambao ni moja ya miji miwili tu inayoshikiliwa na waasi.


Msemaji wa jeshi Philip Aguer kipingamizi cha mwisho ambacho  kilikua ni kifaru kilichokua kinalinda daraja la kuingia katika mji huo. Hata hivyo walifanikiwa kukidhibiti saa 14:30 kwa majira ya huko.

Kiongozi wa waasi Riek Machar ameiambia AFP kuwa vikosi vyake vimeondoka ili tu kutunza amani kwa wananchi ila wameapa kuendeleza mapigano.

Mkuu wa kutunza amani wa UN anasema machafuko hayo yameua watu wasiopungua 1,000.

Mazungumzo ya kutuliza mapigano katika mji wa jirani huko Ethiopia yamesimama.


Endelea hapa kwa taarifa zaidi.

Chanzo www.bbc.co.uk

Friday, January 10, 2014

RAISI WA MPITO WA JAMHURI YA AFRICA YA KATI AJIUZULU


Michel Djotodia rahisi wa mpito wa CAR

Raisi wa mpito wa jamhuri ya Afrika ya kati Michael Djotodia amejiuzulu katika mkutano wa kilele uliokua na lengo la kumaliza mapigano ambayo yameikumba nchi..

Mkutano wote wa mpito unahudhuri mkutano huko Chad ulioitishwa na Wakuu wa nchi.

Michael Djotodia ni rais wa kwanza muislam wa Jamhuri wa Afrika ya Kati aliyepata madaraka mwaka jana.

Toka Disemba na kuwasili zaidi kwa watunza amani na vikosi vya Ufaransa, 
watu 1,000 wamepoteza maisha katika mapigano ya kiitikadi.

Vitongoji vingi vimeteketezwa na mwishoni mwa mwezi uliopita idadi ya watu ambao wamekimbia makazi ya imeongezeka kwa mara mbili ukihisha karibia nusu ya wale ambao wanaishi katika mji mkuu wa Bangui.

Kumekua na matukio ya furaha kwa watu baada ya kutolewa tangazo hilo huko Chad.

Carine Gbegbe, ambaye amekua akiishi katika kambi ya watu wasiokua na makazi, amekiambia chanzo husika, "Hatimaye tupo huru. Tunaelekea kurudi nyumbani".

Vifaru vya Ufaransa haraka vilipelekwa ikulu.

Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian amesisitiza mbadala kwa bw. Djotodia ufanyike "haraka iwezekanavyo".



Tuesday, January 7, 2014

UMASIKINI NA NJAA NDANI YA AFRIKA YETU.

       Katika hali isio ya kawaida watu wengi tunajiuliza maswali mengi kama haya;
i) Kwanini Afrika ni masikini?
ii) Inawezekana vipi A­­­­­frika kuwa masikini huku ina rasilimali za kutosha?
iii) Mbona viongozi wengi wa Afrika wana hodhi mali nyingi ugaibuni hali ya kuwa watu wanaowaongoza ni masikini?.

Haya ni baadhi ya maswali kati ya mengi ambayo watu hujiuliza katika vichwa vyao. Kona ya Abfafrica, inataka leo ijikite kwenye suala hili ilikuweza kupatia ufumbuzi wa haya masuala yanayo tukabili katika maisha yetu ya kila siku. Tafsiri ya umasikini ina uwanja mpana katika fikra za watu mbalimbali hususani waliokuwa bobezi katika masuala ya lugha hii adhimu ya kiswahili.

Umasikini ni hali ya ukosefu wa mahitaji muhimu ya binadamu au ya lazima kwa lugha nyingine kama vile chakula, maji masafi, huduma bora za afya, mavazi na hata nyumba kutokana na kukosa uwezo wa kuvipata au kununua kwa ukosefu wa kipato.

Kona ya Abfafrica haina lengo la kulaumu kama ilivyo desturi ya watu walio wengi bali ina madhumuni ya kuelimisha jamii kama ilivyo desturi yetu waAfrika, ili kuweza kuondokana na vikwazo hivi vikubwa vya kimaisha.

Ukipitia vyanzo mbalimbali vya habari kuna takwimu zimetolewa na shirika la chakula duniani maarufu kama (FAO) zinaonesha kwa jinsi gani bara la Afrika linavyokumbwa ya watu wenye njaa na umasikini. Kwa upande wetu wa Afrika idadi imeongezeka kutoka watu millioni 175 hadi millioni 239, vilevile idadi ya watu millioni 20 iliongezeka huku takwimu ikionesha asilimia 2% inaongezeka kila mwaka hii ni taarifa ya mwaka (2012).

Njaa na umasikini ni vitu ambavyo vinashabihiana kwa kua umasikini huleta njaa na njaa vilevile huleta umasikini.

Kona ya Abfafrica imebaini sababu za umasikini na njaa, ukosefu wa uchumi imara ambao unapelekea wimbi kubwa la ukosefu wa ajira hususani kwa vijana wa Afrika imekuwa ni wimbo wa taifa kwao vilevile hupelekea bara la Afrika kuwa tegemezi kwa mataifa ya magharibi.

Matokeo ya hili ni serikali nyingi za Afrika zinakutana na mashariti makubwa na umasikini unazidi kushika kasi, vilevile vita vya wenyewe kwa wenyewe ndio chanzo kingine cha njaa na umasikini kwa kua watu wanakosa muda wa kuzalisha. Akina mama na watoto ndio wanaathirika kwa kiwango cha juu na hupelekea miji kuwa magofu, idadi ya watu inapungua kutokana na vifo vinaongezeka.


Angalia ndugu zetu wa Sudan ya kusini wanavyo pata shida, ukosefu wa miundombinu katika nchi za Afrika sehemu kubwa ya maeneo ya vijiji katika bara hili hakuna huduma nzuri za barabara za kiwango cha lami, uhaba wa reli na hata vivuko imara angalia mfano wa nchi kama Mali, Burkina Fasso, Sudani ya kusini, Jamuhuri ya Watu wa Afrika ya kati, DRC kongo, Tanzania nk, watu wanapata shida za usafiri na mawasiliano ambayo ni katika vyanzo vikuu vya kiunua kwa haraka uchumi ndio maana tunazidi kuwa masikini wa kupindukia. Mabadiliko ya tabia nchi na uharibifu wa mazingira inapelekea maeneo mengi ya Afrika kukumbwa na njaa pamoja na umasikini usio malizika.

Imeandaliwa na kona ya Afrcan Brotherhood Foundation.

One Blood, One Love, One Africa forever!!!

Monday, January 6, 2014

RAISI WA SUDAN YUPO JUBA KWA MAZUNGUMZO.

Raisi wa Sudan Omar Al Bashir amewasili katika mji wa Juba kwa ajili ya mazungumzo yake na raisi Salva Kiir juu ya mzozo na Sudan ya kusini.

Watu wasiopungua 1,000 wameuliwa toka mzozo ha uanze tarehe 15 December na watu wanaokaribia 200,000 wamehama makazi yao.

Kupotea kwa amani kulianza baada ya raisi wa Sudan wa kusini kumshuku Mr. Machar kwa kujaribu ufanya mapinduzi ambayo yeye anakataa.

Mapigano yamekua yakiendelea wakati mazungumzo yanashika nafasi, kama Alastair Leithead anavyo ripoti.

Kwa taarifa zaidi bofya hapa.

Friday, January 3, 2014

MAZUNGUMZO YA KUSITISHA AMANI YAMEANZA HUKO ETHIOPIA

Hospitali ya kijeshi ya Juba wagonjwa Zaidi ya 1000 katika jengo lenye vitanda 130 tu.
 

Mazungumzo ya kusitisha mapigano yameanza katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa.


Taarifa Zaidi:
Negotiators for the government and rebel sides have been meeting mediators but have not yet met face-to-face.
Meanwhile, the US has announced a "further drawdown" of its embassy staff in South Sudan because of the conflict.
At least 1,000 people have died since fighting erupted between supporters of President Salva Kiir and those of his sacked deputy Riek Machar last month.
.
More than 180,000 people have been displaced, and aid workers say many are living without shelter, clean water and sanitation.
.
What began as a power struggle between President Kiir and Mr Machar has taken on the overtones of an ethnic conflict, correspondents say.
.
 
Evacuation flight
 
Delegates from both sides began arriving in the Ethiopian capital on Wednesday but talks were delayed until the full negotiations teams had arrived
 
Ethiopia's foreign ministry announced in a statement on Friday that negotiations had started
 
The BBC's Emmmanuel Igunza in Addis Ababa says the rival negotiating teams are in the same hotel but are currently in talks only with mediators
 
The mediators are preparing the ground for what they hope will be direct talks later on Friday or into Saturday, he adds.
 
Observers have said the discussions are likely to be complicated, as the two sides will have to agree on a mechanism to monitor a ceasefire.
 
Mr Machar refused to stop fighting ahead of the talks. Mr Kiir has already ruled out any power-sharing arrangement with his rival in the longer term.
 
Meanwhile, the US state department said it had ordered a "further drawdown" of its embassy staff in Juba "because of the deteriorating security situation". For more info visit here
 

Thursday, January 2, 2014

HOTELI IMELIPULIWA NA MAGARI MAWALI YALIYOKUA NA MABOMU HUKO MOGADISHU NCHINI SOMALIA.

Magari mawili yaliyokua na mabomu yamelipuka nje ya hoteli katika mji mkuu wa Somali, Mogadishu na kuua watu wasiopungua 10.

Emily Thomas wa BBC ameripoti kuwa Al Shabaab wamekiri kuhusika na shambulio hilo.

Milipuko ilitokea katika hoteli ya Al Jazeera ambayo wanasiasa wengi wa kisomali na wageni hufikia

Ripoti zinasema milipuko ilitokea na kufuatiwa na majibizano ya risasi kati ya security forces na washambuliaji.

Alshabaab ambao walifukuzwa mjini Mogadishu mwaka 2011 walifanya shambulio hilo. Wanamgambo hao bado wanadhibiti maeneo mengi ya kati na kusini mwa nchi na bado wanatekeleza mashambulio katika mji kuu.

Kwa taarifa zaidi endelea  hapa.

Chanzo www.bbc.co.uk.

Wednesday, January 1, 2014

HABARI YA KUSIKITISHA, WAZIRI WA FEDHA DK. WILLIAM MGIMWA AFARIKI DUNIA

Dr. William Mgimwa


Taarifa ya kuaminika iliyoifikia blog hii kutoka nchini Afrika kusini, inaeleza kua waziri wa fedha, Dr. William Mgimwa (pichani) amefariki dunia leo katika hospitali ya Mediclinic Kloff alopokua amelazwa kwa matibabu.
Dr. William Mgimwa alikua akisumbuliwa na maradhi ya presha kwa muda mrefu.
Mungu aiweke roho yake mahala pema peponi....AMINA.
Taarifa kamili itawajia hivi punde.

Sudan Kusini wakubali mazungumzo

 Sudan Kusini wakubali mazungumzo


Pande mbili zinazopigana katika mgogoro wa Sudan Kusini zimekubali kukukatana nchini Ethiopia kwa ajili ya mazungumzo ya amani, lakini kiongozi wa waasi, Riek Machar, ameiambia BBC kuwa hatasitisha mapigano dhidi ya majeshi ya serikali. Endelea hapa.

Pia amesema majeshi yake yametwaa tena mji muhimu wa Bor kutoka majeshi ya serikali -- lakini madai haya hayajathibitishwa.
Waasi waliushambulia mji huo saa chache kabla ya kumalizika kwa muda uliwekwa na viongozi wa Afrika Mashariki, kwa kuzitaka pande zinazopingana nchini Sudan Kusini kukubaliana kumaliza uhasama kati yao -- au wakabiliwe na majeshi ya nje kwa kuingilia kati mgogoro huo.
Bwana Machar awali alikaririwa akisema asingeingia katika mazungumzo ya amani hadi hapo washirika wake wa kisiasa wanaoshikiliwa na serikali watakapoachiliwa huru.

Mapigano kati ya waasi na askari watiifu kwa Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini, yameenea nchini kote katika kipindi cha wiki mbili zilizopita.