Sunday, January 19, 2014

MGOGORO WA JAMHURI YA AFRICA YA KATI: MIILI YACHOMWA HADHARANI

Thomas Fessy akiripoti kutoka Bangui: Kutokuwepo kwa serikali,
sasa magenge yenye hasira yanaongoza mitaa

Genge la wakristo limewaua na kuwachoma waislam wawili huko Bangui, Jamhuri ya Afrika ya Kati. Hii ni katika mzozo wa kidini unaoendelea.

Genge hilo la majambazi limeiambia BBC kwamba litaendelea kuwaua waislam katika eneo lao.

Majeshi ya Umoja wa Afrika na Ufaransa yanajitahidi kudhibti hali ya mgogoro huo wa kiitikadi za kidini ambao ulizuka mara baada ya kundi kubwa la waasi wa kiislam kuchukua na kudhibiti nchi.

MP wanaelekea kuchagua rais wa mpito ifikapo Jumatatu wiki moja baada ya kiongozi wa waasi Michael Djotodia kuachia madaraka.

Rais huyu alitwaa madaraka baada ya kundi lake la waasi kuipindua nchi mwezi Machi mwaka jana.

Mapinduzi haya yalipelekea kuibuka kwa mgogoro wa kiitikadi za kidini kati ya wakristo wengi na waislam ambao ni wachache.

Bwana Djotodia alijiuzulu tarehe 11 January baada ya kushindwa kutuliza machafuko.

Ingawa ilionekana machafuko kama yanatulia baadaya kujiuzulu lakini imeripotiwa kutokea vurugu zaidi baada ya wiki kupita.

Ijumaa, wakala wa msaada wa afya wamesema kuwa watu wasiopungua 22 wameuliwa katika msafara wa kuwahamisha waislam kulekea Cameroon. 
Watoa msaada wa afya wakiharakisha kuiondoa miili ya waislam waliochomwa.

Genge hilo la wakristu lilimwambia Thomas Fessy wa BBC kuwa wanalipiza kifo cha mkristu mwenzao kilichotokea usiku wake. Haijulikani kama walio uawa wanahusika au wamekua walengwa kwa sababu tu ni waislam.

Baraza la Umoja wa Mataifa limethibitisha kupelekwa kwa vikosi vya Ufaransa huko CAR katika mpango wa kurejesha hali ya utulivu na hatimaye kufanyika uchaguzi kabla ya mwaka 2015.

Jumapili, bunge la mpito limetoa orodha ya wagombea nane wa urais wa mpito.

Maofisa wanasema wagombea wametimiza vigezo, mfano, hawatakiwi kuwa wanachama wa  kundi la kivita na wawe hawajawahi kufanya kazi na Djotodia wala kundi lake la waasi wa Seleka.

Katika wagombea hao yupo Meya wa Bangui na watoto wawili wa marais wa kabla, Sylivian Patasse na Desire Kolingba.




No comments:

Post a Comment