Saturday, January 11, 2014

Mgogoro wa Jamhuri ya Afrika ya Kati: Wageni wasiokuwa na makazi kuondolewa.

Kambi ya muda inayohifadhi watu wanaokadiriwa kufikia 100,000 wasiokua na makazi katika uwanja wa ndege wa Mpoko, Bangui.

Awamu ya kwanza ya kuhamishwa kwa dharura kwa maelfu ya wageni waliokimbia machafuko katika Jamhuri ya Afrika ya Kati imeanza leo Jumamosi.

Shirka la kimataifa la uhamiaji (IOM) limesema litaanza kuwasafirisha watu 800 wa Chad  kutoka kwenye kambi ya muda huko Bangui.

Raisi wa mpito wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Michael Djotodia alijiuzulu Ijumaa kutokana na maigano kati ya wapiganaji wa kiislam na kikristo.



Bwana Djotodia, raisi wa kwanza muislam, aliyepata madaraka mwaka uliopita. Toka hapo 20% ya watu wamelazimika kukimbia ili kuepuka vurugu.

Watu wasiopungua 1,000 wamefariki toka machafuko yaanze mwezi December.

Kwa sasa umoja wa Afrika ina watunza amani 4,000 ndani ya nchi. Sambamba na hilo Ufaransa inapeleka vikosi 1,600 kwenda kujaribu kurejesha amani.



Kiongozi wa umoja wa mataifa ametoa tahadhari ya kutokea majanga makubwa ya kiubinadamu.

Bofya hapa kwa taarifa zaidi.

Chanzo BBC.

No comments:

Post a Comment