Saturday, January 11, 2014

Mgogoro wa Sudani ya Kusini: UN yatoa wito kwa serikali kuwaachia wafungwa

Baraza la usalama la umoja wa mataifa limemuomba rais wa Sudani ya Kusini Salva Kiir awaachie wafungwa wa kisiasa ili kusaidia katika kuhitimisha machafuko yanayoendelea. 



Kiongozi wa waasi, Riek Machar, anataka watu kumi na moja waachiwe huru kabla ya makubaliano ya amani kufanyika.

Vikosi vya Machaar vinaonekana kuzidiwa nguvu baada ya kupoteza mji wa Bentiu na kuchukuliwa na majeshi ya serikali katika siku ya Ijumaa.

Serikali inasema inapeleka maelfu ya vikosi ili kudhibiti Bor - mji mkubwa na wa mwisho unaodhibitiwa na vikosi vya waasi.

Machaar, makamu wa raisi aliyefukuzwa kazi, ameonesha nia ya kuendelea kudhibiti mji huo ambao upo umbali wa km 200 kaskazini mwa mji mkuu wa Juba.



Akiongea na AFP kwa simu, wakala wa habari, aliyejaribu kueleza tukio la waasi kupoteza mji huo:
"Ilikua ni kuepuka mapigano katika mitaa na kulinda maisha ya raia," alisema.

Msemaji wa jeshi  Philip Aguer amesema baadhi ya wapiganaji wa pande zoe wamepoteza maisha.

Pamoja na serikali kuingia katika mji huo, maelfu ya watu wameihama Bentiu, na maelfu kadhaa ya watu wametafuta hifadhi katika kambi ya UN hapo mjini.

Kwa taarifa zaidi endelea hapa.

Chanzo www.bbc.co.uk/news

No comments:

Post a Comment