Toka Disemba na kuwasili zaidi kwa watunza amani na vikosi vya Ufaransa,
watu 1,000 wamepoteza maisha katika mapigano ya kiitikadi.
Vitongoji vingi vimeteketezwa na mwishoni mwa mwezi uliopita idadi ya watu ambao wamekimbia makazi ya imeongezeka kwa mara mbili ukihisha karibia nusu ya wale ambao wanaishi katika mji mkuu wa Bangui.
Kumekua na matukio ya furaha kwa watu baada ya kutolewa tangazo hilo huko Chad.
Carine Gbegbe, ambaye amekua akiishi katika kambi ya watu wasiokua na makazi, amekiambia chanzo husika, "Hatimaye tupo huru. Tunaelekea kurudi nyumbani".
Vifaru vya Ufaransa haraka vilipelekwa ikulu.
Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian amesisitiza mbadala kwa bw. Djotodia ufanyike "haraka iwezekanavyo".
No comments:
Post a Comment