Wednesday, January 22, 2014

PIGO KUBWA KWA AFRIKA BAADA YA KUMPOTEZA MWANAHABARI WETU MAHIRI, KOMLA DUMOR

Komla Dumor

Imeripotiwa; Mwanahabari wa BBC TV, Komla Dumor 41, amefariki ghafla katika nyumba yake iliyopo London.

Ni mzaliwa wa Ghana, alikuwa ni mtangazaji wa habari za BBC za dunia haswaa katika habari za Afrika.

Mtangazaji huyu alikua ni maarufu duniani, alijiunga na BBC kama mrusha matangazo ya redio mwaka 2006, baada ya kuwa mwanahabari kwa muda wa muongo mmoja huko Ghana.

Rais wa Ghana ametangaza kupitia Twitter kwamba nchi yake imepoteza moja ya "mabalozi mahiri".

Mkurugenzi wa habari za dunia BBC Peter Horrocks amemuita Komla Dumor mwongozo wa wanahabari wa Afrika  ambaye atakumbukwa sana kwa mchango wake.

"Alidhamiria kuelezea habari ya Afrika kama ilivyo" Bwana Horrocks alisema katika tamko.

"Furaha na nguvu ya Afrika huonekana kuongezeka katika kila habari aliyo eleza Komla".

"Ndugu na marafiki katika Afrika yote watakuwa na huzuni kama tulivyo sisi katika habari hii ya kuhuzunisha".

BBC imekua ikielewa kwamba Komla alikuwa akiumwa ugomjwa wa moyo.

Katika jarida la New African's magazine, la Novemba 2013, Komla alikua katika orodha ya watu 100 wenye ushawishi katika bara la Afrika. Lilisema "Komla amekuwa ni uso wa Afrika katika habari za ulimwengu na amekua na ushawishi mkubwa katika jinsi gani tunaifikia Afrika.

Komla Dumor alikua na ujuzi na mbinu za kuvutia katika utangazaji.
 James Harding, mkurugenzi wa habari na mambo ya sasa, akiongelea "jukumu pekee la Komla Dumor katika kuifikia Afrika". Alitumia uelewa, ujasiri wa hali ya juu, furaha yenye kuvutia na mvuto kwa watu katika kazi yake.

Komla Dumor alizaliwa tarehe 3 Octoba 1972 huko Accra Ghana.

Alipata bachela ya socialogy na saikolojia katika chuo kikuu cha Ghana na masta ya public administration katika chuo kikuu cha Havard.

Alipata tuzo ya mwana habari bora wa Ghana mwaka 2003 na miaka miwili baadae alijiunga na BBC.

Kuanzia hapo mpaka alikua akitangaza kipindi cha Network Afrika katika redio ya BBC world service kabla hajajiunga katika kipindi cha World Today

Komla Dumor akitangaza kipindi cha African Business Report mwaka 2009.

Mwaka 2009 Komla akawa mtangazaji wa kwanza wa kipindi cha African Business report katika habari za ulimwengu za BBC.  Pia alikua mtangazaji wa kipindi cha Focus on Africa na alifanya kazi hiyo siku moja kabla hafariki.

Alitembelea sehemu nyingi za Afrika akikutana na wajasiriamali maarufu na kuripoti mambo ya biashara yanayo endelea katika sehemu mbalimbali za baa la Afrika.

Alifanya mahojiano na wageni wa hadhi ya juu kabisa hii ni pamoja na Kofi Annan na Bill Gates.

Mwezi uliopita, alishughulika katika kutaripoti mazishi ya rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, ambaye alimwelezea kama "moja ya watu maarufu katika historia ya sasa."

Alifanya matangazo ya moja kwa moja ya matukio makubwa kama kombe la dunia la mwaka 2010 huko Afrika Kusini, mazishi ya Kim Jong-il, kuachiwa kwa mwanajeshi wa Izrael Gilad Shalit, na ndoa ya mtoto wa mfalme, William na Kate Miidleton.

Katika mjadala wa 2013 uliochapishwa mwezi jana, Dumor alisema kufariki kwa Mandela ni "moja ya vipindi vitakavyobaki na yeye".

"Kuripoti mazishi kwa mimi kumekua na kutaendelea kuwa tukio la kipekee. Taliangalia tukio hili kwa hali ya huzuni na kwa shukrani na heshima. Najiona mwenye bahati kuwa shahidi katika sehemu ile ya historia ya Mandela".

"Hajawahi kuterereka!"

Kukutana n Komla Dumor kwa mara ya kwanza mwaka 2007, mkuu wa watoa habari wa kimataifa Lyse Doucet algundua ni kwa jinsi gani mwanahabari huyo alionekana kwake.

Hajawahi kuwa muoga katika kuuliza mwaswali magumu, pia alipenda kufurahi na wengine, alisema.

Aliongeza kuwa Komla Dumor alikua na vitu vingi alivyokua napenda kama soka, imani yake na familia yake.

Ameacha mke na watoto watatu. 



No comments:

Post a Comment