Wednesday, January 29, 2014

SUDANI YA KUSINI: Machar asema tuhuma za mipango ya mapinduzi hazina "mashiko".

Ramani ya vita Sudani ya Kusini.

Kiongozi wa waasi Sudani ya Kusini ameiambia BBC tuhuma za mapinduzi juu yake na baadhi ya washirika wake hazina mashiko.

Bwana Machar ambaye kwa sasa yupo katika harakati za kukimbia amesema anategemea wajumbe katika mgogoro huu watahakikisha washirika wake wanne waliofungwa wanaachiwa.

Wachambuzi wanasema suala hili linatishia mkataba wa amani ulio sainiwa wiki iliyopita.

Mwezi Disemba Maofisa walitangaza  kwamba wanasiasa saba wanatuhumiwa kufanya jaribio la mapinduzi.

Mwanzo ulikua ni mgogoro wa kisiasa kati ya rais Salva Kiir na makamu wake wa zamani Bwana Machar tarehe 15 Disemba.

Kuanzia hapo vurugu zilianza zikapelekea vita kubwa na imeripotiwa kutokea mauaji ya kikabila.

Wanasiasa saba maarufu waliokuwa wakikiongoza chama cha SPLM walikamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi mara tu baada ya madai ya kutaka kufanya mapinduzi.

katika wanasiasa hao wanne wanatuhumiwa kufanya mapinduzi na wengine saba wameachiwa katika mamlaka za Kenya ambapo walionekana wakiwa na Rais wa Kenya Uhuru Kenyata katika mkutano wa habari hapo siku ya Jumatano.

Zaidi ya watu 646,000 wamepoteza makazi toka mapigano yaanze mwezi Disemba.

No comments:

Post a Comment