Saturday, January 11, 2014

Vikosi vya Sudani ya kusini vimefanikiwa tena kudhibiti mji muhimu wa Bentiu.

Andrew Harding wa BBC ameripoti kuwa ineonakana Bentiu ilidhibitiwa kutoka kwa waasi kukiwa na "upinzani mdogo tu."

 Jeshi la Sudani ya Kusini linasema wamefanikiwa kudhibiti tena kitovu cha mafuta Bentiu, mji ambao ni moja ya miji miwili tu inayoshikiliwa na waasi.


Msemaji wa jeshi Philip Aguer kipingamizi cha mwisho ambacho  kilikua ni kifaru kilichokua kinalinda daraja la kuingia katika mji huo. Hata hivyo walifanikiwa kukidhibiti saa 14:30 kwa majira ya huko.

Kiongozi wa waasi Riek Machar ameiambia AFP kuwa vikosi vyake vimeondoka ili tu kutunza amani kwa wananchi ila wameapa kuendeleza mapigano.

Mkuu wa kutunza amani wa UN anasema machafuko hayo yameua watu wasiopungua 1,000.

Mazungumzo ya kutuliza mapigano katika mji wa jirani huko Ethiopia yamesimama.


Endelea hapa kwa taarifa zaidi.

Chanzo www.bbc.co.uk

No comments:

Post a Comment