Magari mawili yaliyokua na mabomu yamelipuka nje ya hoteli katika mji mkuu wa Somali, Mogadishu na kuua watu wasiopungua 10.
Emily Thomas wa BBC ameripoti kuwa Al Shabaab wamekiri kuhusika na shambulio hilo.
Milipuko ilitokea katika hoteli ya Al Jazeera ambayo wanasiasa wengi wa kisomali na wageni hufikia
Ripoti zinasema milipuko ilitokea na kufuatiwa na majibizano ya risasi kati ya security forces na washambuliaji.
Alshabaab ambao walifukuzwa mjini Mogadishu mwaka 2011 walifanya shambulio hilo. Wanamgambo hao bado wanadhibiti maeneo mengi ya kati na kusini mwa nchi na bado wanatekeleza mashambulio katika mji kuu.
Kwa taarifa zaidi endelea hapa.
Chanzo www.bbc.co.uk.
No comments:
Post a Comment